Wednesday 13 July 2016

UTOAJI MIMBA (ABORTION) NA "KUPATA WATOTO WENYE AKILI"

NANI KAMA MAMA?

Constantine Ntanguligwa(MD student Muhimbili university of health and allied sciences) 
2230hrs 13th July 2016

Kuna msemo maarufu wa nani kama mama? Ni kweli hatukatai kuwa hakuna kama mama. Je wakina mama/dada, mnajua nguvu mliyonayo katika kuhakikisha mnaipatia dunia kiumbe kilichochema?

TUTAJIBU MASWALI  MAKUBWA YAFUATAYO MWISHONI:
  1.          UTOAJI MIMBA UNA HASARA GANI KIAFYA?
  2.          SHERIA YA UTOAJI MIMBA INAAGIZA VIPI?
  3.          NI SEHEMU GANI ZA NCHI ZINAONGOZA KWA UTOAJI MIMBA?
  4.         MCHANGO WA MAMA KATIKA UBORA WA MTOTO ATAKAYEZALIWA AKIBEBA UJAUZITO

Karibu tuzungumze,

Utoaji mimba (abortion) ni pale mimba inapotoka bila kutimiza mda wake sahihi wa mama kujifungua (miezi tisa) kama tulivyozoea kusema. Hii inaweza kuwa aina mbili:
  1. ·         Mimba kutoka yenyewe
  2. ·         Mimba kutolewa kwa makusudi

Ni wadada wangapi tumeshawahi kujikuta kwenye kipindi ambapo tumepata mimba bila kukusudia na kujiuliza niitoe au nisiitoe kwasababu mbalimbali?
Ni wakaka wangapi tumeshawahi kujikuta kwenye kipindi ambacho mpenzi wako anapata mimba ambayo hauko tayari kuilea? Na kufanya uamuzi wa haraka wa kumwambia aitoe nay eye akakataa?
Huku mtaani kwetu mara utasikia jamaa wakimshauri mwenzao, “ah ukitaka kuitoa, majani ya chai mbona fasta tu?” Mara ngapi wengine wamekuwa wakitumia spoku na chelewa kujiingiza kwenye njia za uzazi kujaribu kuitoa mimba? Je ni kweli tunajua tunachokifanya?

Katika Muhimbili University of health and allied sciences scientific conference mwaka HUU 2016 mtalaamu mmoja Prof. Muganyizi (mtalamu wa afya ya kina mama) alieleza kwa kina kuhusu hili. Alisema:
·         Kwa nchi yetu Tanzania, UTOAJI MIMBA UNARUHUSIWA PALE TU AMBAPO AFYA YA MAMA IKO HATARINI. Swali ni je, nani wa kuitoa mimba hiyo?

·         Tanzania katika mimba kumi, nne hazikutarajiwa.
·         Kati ya hizo zisizotarajiwa 15% hutolewa kwa makusudi na 5% huishia kutoka zenyewe.
IMAGINE IF IT WAS YOUR OWN MOM WHO DID THIS TO YOU, WHERE COULD YOU BE?!!!!
·         Mwaka 2013 watu tafiti ilifanywa kwa watu milioni moja, 39% mimba zilitolewa kwa makusudi na kanda ya ziwa ndo wanaongoza kwa utoaji mimba 52%.

Kinachotisha hapo ni kwamba wengi 40% waliotoa mimba wanaishia kupata matatizo makubwa sana ya kiafya kama:
  •         Kupoteza maisha kwa kupoteza damu nyingi mtoto anapotoka
  •          Kupasuka kwa mfuko wa uzazi hivyo kushindwa kuzaa tena
  •          Kuharibu njia za uzazi (cervix)
  •          Matatizo ya kisaikolojia  n.k 
Hii hutokana na utoaji mimba kufanywa na watu wasiokuwa na ujuzi. Tafiti inaonesha, utoaji mimba ukifanywa na mtalamu wa afya hatari ya kupata matatizo inapungua sana. Angalizo ni kwamba usitumie hii kama faida uende kumuhonga daktari atoe mimba. Kwa nchi yetu kama nilivyosema hairuhusiwi na kuna sharia kali kama ifuatavyo: Nanukuhu

,” Under the Penal Code, section 230, termination of pregnancy is lawful where it is done to preserve the life or health of the pregnant woman. 150 – Any Person who, with intent to procure miscarriage of a woman, whether she is or is not with child, unlawfully administers to her or causes her to take any poison or other noxious thing, or uses any force of any kind, or uses any other means whatever, is guilty of a felony, and is liable to imprisonment for fourteen years. 151- Every woman being with child who with intent to procure her own miscarriage unlawfully administers to herself any poison or other noxious thing, or uses any force of any kind, or uses any other means whatsoever, or permits any such thing or means to be administered or used to her, is guilty of a felony, and is liable to imprisonment for seven years. 152- Any person who unlawfully supplies to or procures for any person anything whatsoever, knowing that it is intended to be unlawfully used to procure the miscarriage of a woman, whether she is or is not with child, is guilty of a felony, and is liable to imprisonment for three years. Section 219 (1) - Subject as hereinafter in the subsection provided, any person who with intent to destroy the life of a child capable of being born alive, by an wilful act causes a child to die before it has an existence independent of its mother, shall be guilty of the felony of ‘child destruction’, and shall be liable on conviction to imprisonment for life; Provided that no person shall be guilty of an offence under this section unless it is proved that the act which caused the death of the child was not done in good faith for the purpose only of preserving the life of the mother.”

Who knows what the child would become? Another Bilget or another Doctor?

Ni kweli kila mtu anatamani kuwa na mtoto mwenye akili za darasani. Mtoto msikivu. Mtoto mzuri ambapo akitajwa utasema kwa haraka sana “kuwa huyo ni mwanangu jamani.” Wengi na tunaamini kuwa vitu hivi hutokea tu kwa kufuata historia za ukoo. Ni kweli hatukatai lakini kama mama na baba kuna mchango mkubwa sana unaoweza kutoa/kutengeneza mazingira ya kupata watoto wa aina hii tunaowataka.

Kwa ufupi. Safari nzima ya uzazi tunaigawa sehemu tatu (trimester).
·         I- wiki ya 1 mpaka ya 13
·         II- wiki ya 14 mpaka ya 26
·         III- wiki ya 27 mpaka ya 39
Safari nzima ya wiki kama 39 hivi (miezi tisa)   
  •       Stage I acha kabisa vilevi, sigara , vipodozi , Mionzi mikali (kama X rays) na Vichafuzi mazingira vyenye nguvu
  • *      Stage III kuwa makini na nguo unazovaa, kwa ujumla ulinde tumbo lako lisipate usumbufu wowote kwasababu stage hii physical injuries ni hatari zaidi.
  • *      Jilinde, kula vizuri kwasababu kila unachokula na kunywa mtoto naye anakula na kunywa hicho hicho.
  • *      Tembelea wodini walau mara moja kila mwezi.
Nasisi wakina Baba tuzingatie wapenzi wetu wanafuata haya na kuhakikisha hatui chanzo cha kuleta matatizo kwa mama kwasababu na mtoto ataguswa na matatizo hayo hayo.
Zingatieni haya na mtoto wenu atakua mwenye afya nzuri na aliyelelewa vizuri tangu tumboni mwa mama.

Vifo vya kina mama na watoto wenye umri chini ya miaka mitano ni vingi mno. KAMWE USIKUBALI KUJIFUNGULIA NYUMBANI. OKOA MAISHA YA MTOTO. HAKIKISHA SAFARI YAKE YA KUJA DUNIANI INAKUA NJEMA NA SALAMA.

KULINDA AFYA YA MAMA NA MTOTO NI MIMI NA WEWE.

6 comments: