Wednesday 27 July 2016

HEADACHE (MAUMIVU YA KICHWA)

HEADACHE (MAUMIVU YA KICHWA)
Constantine Ntanguligwa(MD student Muhimbili university of health and allied sciences)
 2130hrs 27th July 2016

Karibu tuzungumze:

Ni siku nyingine mtu wangu wa nguvu. Leo nakuletea makala kuhusu Maumivu ya kichwa. Ni kitu ambacho kimezoeleka na huwa sehemu ya maisha yetu mda mwingine. Mara nyingi tumekuwa watumwa wa dawa za kupunguza maumivu(pain killers) na kwa lugha ya kitaalamu "analgesics". Labda nikwambie tu kuwa hatushauriwi kunywa dawa za kupunguza maumivu angalau bila kuandikiwa ya daktari. Hii ni kwasababu nyingi za kiafya kama;

  • Dawa hizi hupunguza maumivu na huweza kukudanganya kuwa umepona kumbe bado. Hii ni hatari hasa kama tatizo linalosababisha maumivu hayo ni kubwa sana kama kupata uvimbe kwenye ubongo. 
  • Dawa hizi huweza leta vidonda vya tumbo hasa Asprin. 
  • Dawa hizi huweza kusababisha "addiction". Unaweza kujikuta mtumiaji wa dawa za kupunguza maumivu na ukawa mtumwa kama wa dawa za kulevya (addiction, dependance and tolerance). 
  • Ukizidisha dozi inaweza kusababisha kifo. 
Sasa kikubwa tutakachojifunza hapa leo ni aina ya maumivu ya kichwa, ili tuone kuwa kumbe dawa za kupunguza maumivu zinaweza kutudanganya tatizo likawa si kichwa tu. Ntaongelea baadhi tu na nitaongelea kwa juu juu lakini jinsi gani inasababisha mpaka unapata maumivu ni maswala ya kitalamu( beyond normal understanding). 

1.MIGRANE HEADACHES
Migraine headaches often begin with early symptoms indicating the onset of an attack or a disease such as nausea (kichefuchefu), loss of vision in part of the field of vision(kupungua uwezo wa kuona), visual aura and other types of sensory hallucinations(kuhisi vitu vipo kumbe havipo). Ordinarily, these symptoms begin 30 minutes to 1 hour before the beginning of the headache.

Moja ya nadharia ni kwamba huwa inasababishwa na stress, mvutano na msongo wa mawazo kwa mda mrefu. Hutokea mara nyingi kwa wanawake.

2. Headache attributed to trauma or injury to the head and/or neck:
Hii husababishwa na kujigonga sehemu, kulalia shingo vibaya au kujiumiza kichwani au shingoni kwa namna yoyote ile mfano baada ya Ajali. Inaweza kuwa umeumiza kitu ndani hivyo ni vema ukahakikisha chanzo chake kikuu.

3.Headache attributed to cranial or cervical vascular disorder
Hii husababishwa na matatizo na mfumo wa damu kwenye kichwa. Inaweza kuwa mishipa ya damu kichwani imevimba (vasculitis), kutofika damu ya kutosha kichwani(ischemia), damu kuvujia kichwani(haemorrhage) hasa bila kukigonga kichwa sehemu au bila ajali yoyote, kutoumbwa katika mfumo wa kawaida(malformation like Fistula au kupanuka mishipa ya damu-aneurysm) n.k.

4. Headache attributed to non-vascular intracranial disorder
Hii husababishwa na matatizo ya ndani ya kichwa pia. Kupata "pressure" iliozidi kiwango(hypertension) kichwani si kwasababu ya damu bali kitu tunaita "cerebral spinal fluid" ambacho ni kimiminika kwenye ubongo, kujaa maji kichwani(hydracephalous), kupungua kwa kiasi cha "cerebral spinal fluid" n.k ya kitaalamu zaidi kama neurosarcoidosis, carcinomatous meningitis na epileptic seizure.

5.Headache attributed to a substance or its withdrawal
Hii hutokea kutokana na matumizi au kuacha ghafla dutu(substance) uliyozoea kutumia sana mfano madawa ya kulevya, pombe na baadhi ya vyakula au vinywaji.

6. Headache attributed to infection
Hii hutokana na maambukizi kwenye kichwa hasa ndani ya kichwa na sehemu zake. Maambukizi haya yanaweza kuwa bacteria, virusi au fungus. Hii huweza pelekea baadhi ya sehemu kuvimba au kufanya kazi isivyotakiwa(abnormal functioning).

7.Headache attributed to disorder of homoeostasis
Hii usababisha na kutokua na uwiano(balance) kwenye systems za kichwa. System zinakuwa zina vitu kuzidi kawaida mfano upungufu wa oxygen inayofika kichwani ambayo inaweza kusababishwa na kwenda urefu wa juu mfano ukipanda milima, ukipanda ndege, wanaoogelea. Pia huweza wapata wajawazito waliokaribu kupata kifafa cha mimba au kifafa cha mimba kinapotokea(eclampsia and pre-eclampsia).

8. Headache or facial pain attributed to disorder of the cranium, neck, eyes, ears, nose, sinuses, teeth, mouth or other facial or cervical structure
Hii yenyewe husababishwa na kiungo chochote kilichopo kichwani. Huweza kuwa macho, pua, fuvu, mdomo au meno. Huweza kuwa uvimbe pia wa vitu hivi. Huenda pia kukawa na kubanwa kwa mishipa ya damu au mishipa ya fahamu(nerves)

9. Headache attributed to psychiatric disorder
Hii huweza sababishwa na matatizo ya kiakili(psychiatric). Matatizo ya kiakili si lazma pale utakapokuwa chizi tu. Hata mwenye msongo wa mawazo, mwenye ulevi(addiction). Huweza kuwa Psychosis ( a mental health problem that causes people to perceive or interpret things differently from those around them. This might involve hallucinations or delusions) au Somatization (tendency to experience and communicate psychological distress in the form of somatic symptoms and to seek medical help for them. More commonly expressed, it is the generation of physical symptoms of a psychiatric condition such as anxiety ).

"Hizi zote ni aina za maumivu ya kichwa. Unaweza kujionea mwenyewe sasa kwanini tunakushauri usinywe dawa za kupunguza maumivu bila ushauri wa daktari. Inafanywa hivi ili tujue chanzo kikuu cha maumivu ya kichwa. Tujue kuwa kichwa ni sehemu nyeti sana kwani ndo mwanzo wa kila kitu mwilini na muamuzi mkuu wa kila kitu mwilini hivyo maumivu ya kichwa si ya kuchukulia masihara."
Nitawapa ushuhuda. Yupo mtu ambaye alikua anapata maumivu ya kichwa na alikua ni mgonjwa wa macho na anavaa miwani. Alipata maumivu ya kichwa mara kwa Mara lakini alichukulia tu ni macho yake tu yanasumbua na akafanya mazoea ya kunywa dawa za kupnguza maumivu. Siku alipozidiwa sana hata kupoteza fahamu na kukimbizwa hospitali ndipo alipogundulika kumbe ana tatizo lingine kichwani na bahati nzuri aliwahi pengine angechelwa kungekuwa na madhara mengine zaidi.

WAHI HOSPITALI MAPEMA /KWA WAKATI PINDI UHISIPO KITU SI CHA KAWAIDA. AFYA YAKO, MAISHA YAKO VIPO MIKONONI MWAKO.

Special aknowledgements :
  • Headache Classification Committee of the International Headache Society (IHS) The International Classification of Headache Disorders, 3rd edition (beta version) 
  • Guyton and Hall Textbook of Medical Physiology, 11ed 
Untill next time.

No comments:

Post a Comment