Monday 25 July 2016

Je, unafahamu wale wote(wahudumu) wanaohusika na matibabu yako hospitali? Je, unafahamu fursa sekta ya Afya?

WAHUDUMU WA AFYA(HEALTH PRACTITIONERS AND HEALTH PRACTICE)
Constantine Ntanguligwa(MD student Muhimbili university of health and allied sciences) 
2230hrs 25th July 2016

Karibu tuzungumze:

Habarini, watu wangu wa nguvu. Leo nakuletea Makala hii:
  • Yenye manufaa kwa watu wote kufahamu watu wa Afya wanaowahudumia.Mara nyingi, tumekuwa tukisema tu doctor asante. Lakini je, tunajua ni watu wangapi wanahusishwa kwenye matibabu yako mpaka unapona? Ni kweli mchango wao unaweza kuwa mdogo kuliko daktari lakini kamwe sehemu yao ni muhimu sana katika sector ya Afya.

  •  Kushawishi wanaojiunga na vyuo kujiunga na sekta za Afya mbalimbali mbali, hivyo wajue fursa zilizopo kwenye sector ya Afya. Ili nchi yetu ipate wahudumu wa kutosha nikifanya reference Vyuo vya Afya mbali mbali nchini. 

Naongelea kwenye degree level. Hii ni kwasababu, watu wengi huchanganya sana na kutowajua ipasavyo watu hawa na pengine kuwadharau. Labda kwasababu tumezoea kuwaona kwenye vituo vya afya mbali mbali (dispensaries) lakini hao ni wale wenye hadhi ya diploma kwenda chini. Mimi ntaongelea wenye hadhi ya degree, ili angalau uone uzito wao. Wenye hadhi hii wengi utawakuta hospitali za wilaya, mkoa mpaka taifa na kimataifa, hivyo ni watu wenye umuhimu mkubwa sana kama ifuatavyo.
   1.  NURSES:

 Opportunities available:
  •          Bachelor of Science in Nursing (BSc N)
  •          Bachelor of Science in Nursing (Management) (BScN Management)
  •          Bachelor of Science in Midwifery (BScM)- wakunga

Mistakanely watu wanadhani nursing ni kwa women tu. Si hvyo. Nurse ni mtu yoyote anaweza kuwa na kazi yake kubwa ni kuhandle caring ya mgonjwa and sometimes wana assist operations. Na mda mwingine kama katika kujifungua kwa kina mama kwa kawaida wao ndo wahusika wakuu.
“Nursing is a profession within the health care sector focused on the care of individuals, families, and communities so they may attain, maintain, or recover optimal health and quality of life. Nurses may be differentiated from other health care providers by their approach to patient care, training, and scope of practice. Many nurses provide care within the ordering scope of physicians, and this traditional role has come to shape the historic public image of nurses as care providers
"Nurses develop a plan of care, working collaboratively with physicians, therapists, the patient, the patient's family and other team members, that focuses on treating illness to improve quality of life. Nurses may help coordinate the patient care performed by other members of an interdisciplinary health care team such as therapists, medical practitioners and dietitians.”(https://en.m.wikipedia.org/wiki/Nursing)
    
  2.PHARMACISTS:
Opportunities: Bachelor of pharmacy

Mistakenly watu wanadhani hawa ndo wale wanaokaa kuuza dawa kwenye pharmacy. It maybe true, some of them stay in the pharmacies but not because they studied to work there but rather just a matter of choice and self employment. Wao ndo wahusika wakuu wa dawa tunazotumia, wakipima uwezo wa kila dawa, madhara yake n.k.
“Pharmacists are healthcare professionals who practice in pharmacy, the field of health sciences focusing on safe and effective medication use. A pharmacist is a member of the health care team directly involved with patient care. Pharmacists undergo university-level education to understand the biochemical mechanisms and actions of drugs, drug uses, therapeutic roles, side effects, potential drug interactions, and monitoring parameters. Pharmacists interpret and communicate this specialized knowledge to patients, physicians, and other health care providers.” (https://en.m.wikipedia.org/wiki/Pharmacist)
         3.   DOCTOR:
Opportunities:
  •         Doctor of Medicine
  •          Doctor of Dental surgery (East Africa ipo Muhimbili University na Nairobi university tu)-Mtaalamu wa meno

Huyu yeye tumemzoea na ndo tunayemjua siku zote na kumuona tunapokwenda hospitali, daktari. Swali ni kwamba kwanini watalamu wa meno huwa wanachukuliwa ni madaktari wa kipekee? Kwa sababu watu hawa husoma miaka mitano na badala ya kuwa madaktari wa kawaida wao wanakuwa watalamu wa meno moja kwa moja. Hapo ndo utakapojua kuwa mwili wa binadamu unahitaji uangalizi na ulinzi mkubwa kwani meno tu yamepewa hadhi ya kipekee.
     
     4. LAB TECHS (wataalamu wa maabara)
Opportunities:
·         Bachelor of Medical Laboratory Sciences in Clinical Chemistry (BMLS Clin.Chem)
·         Bachelor of Medical Laboratory Sciences in Haematology and Blood Transfusion (BMLS Haem.BT)
·         Bachelor of Medical Laboratory Sciences in Histotechnology (BMLS Histotech.)
·         Bachelor of Medical Laboratory Sciences in Microbiology and Immunology (BMLS Micro.Immunol.)
·         Bachelor of Medical Laboratory Sciences in Parasitology and Medical Entomology (BMLS Para.Entomol.)
·         Bachelor of medical Laboratory Sciences General Degree.

Watu hawa ni wataalamu wa maabara. Watu hawa wana kazi kubwa sana. Mfano, pale HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI kuna central pathology lab. Jengo hili linafanya kazi kubwa sana mfano kupima kila aina ya magonjwa kutoka kwenye sampuli za wagonjwa wote wa hospitali ya taifa, huusika kwenye kuchangia damu na kuihifadhi. Hivyo hawa kazi yao ndo itaamua kwa kiasi kikubwa kama alichohisi daktari ni kweli au lah!
So we need these people so much and their work is highly in constant need of specialists in this field.

5.       RADIATION THERAPIST (watalamu wa mionzi)
Opportunities: Bachelor of Science in Radiation Therapy Technology (BSc RTT)

Watu hawa wanaojua umuhimu wao ni wale waliokwisha fanyiwa X-ray, CT-scan, Ultrasound au kutibiwa kansa kwa mionzi. Watu hawa ni wataalamu wa mambo yote katika sekta ya afya yanayohusu mionzi.
Kansa ni tatizo kubwa sana linalotabiriwa kuongezeka kwa kasi sana. Watu hawa kwa kiasi kikubwa husaidia matibabu kwa mionzi katika ugonjwa huu wa hatari sana. Hivyo wanaumuhimu mkubwa sana na wanahajika.

6.       Health Environmentalist (wataalamu wa Afya mazingira):
Opportunities: Bachelor of Science in Environmental Health (BSc. Env. Health)

Watu hawa hawakutani na sisi moja kwa moja lakini wao ndo wahusika wakuu wa mazingira yetu. Kwani magonjwa yanatoka wapi? Si kwenye mazingira yetu? Wao huchunguza mazingira, kufanya tafiti na huweza kutabiri magonjwa mapya na kuangalia namna gani tunaweza kurekebisha mazingira yetu hata mda mwingine kufanya magonjwa kuwa historia. Labda ndo chanzo cha baadhi ya nchi kutokuwa na magonjwa mengine tunayoyafahamu katika nchi zao. Wana mchango mkubwa sana. Ni watu wa NGO’s hawa na opportunities za kutumika na Umoja wa mataifa (UNO).
 Unajua kinga ni bora kuliko tiba. Sasa, ukitibiwa kipindu pindu kwa mfano, halafu usipobadili mazingira na kuyaweka safi itakuwa kazi bure sababu utarudi kwenye ugonjwa ule ule. Hivyo kazi ya watu hawa ni kuhakikisha kuwa ikitokea bahati mbaya umeumwa, usiumwe tena.
Kuna mchanganyiko wa mambo hapa. Kuna wanaosoma Environmental engineering hao sitawagusia kwasababu wao hawajabobea katika mazingira kiAfya, wao ni wahandisi wa mazingira mfano kutafuta namna ya kutengeneza vyanzo rafiki vya nishati na kulinda uchafuzi wa mazingira au kuhakikisha viwanda vinatengenezwa katika teknolojia ambayo haiharibu mazingira.
   
      7. Viungo bandia:(hii inapatikana KCMC tu kwa sasa)
Opportuinities: Orthopaedic Technologists na Prothetist/Orthotist

Watu hawa, kama inavyojieleza hapo, wanahusika katika utengenezaji na utumiaji wa viungo bandia. Kuwapa mazoezi watu waliopata ajali na kuhakikisha wanapewa tiba mbadala hasa inapotokea matatizo ya ulemavu. Kwa ajali hizi za barabarani zinazoendelea hasa bodaboda, hii inaweza kuwa fursa nzuri sana kama utaweza kusoma na kuamua kuanzisha kampuni yako ya viungo bandia kwani hapa nchini sekta hii ipo wazi sana (hajapewa kipaumbele sana na serikali).

Conclussion/Reccomendation: Watu hawa ni wa muhimu sana. Ila huwezi kutambua umuhimu wako mpaka pale watakapokuwa katikati ya maisha yako na kifo. Wanajitoa sadaka sana na wanajiweka katika hatari ya kila namna.
 Hawa ni watu wa kwanza kupata ugonjwa wowote wa maambukizi mapya kutoka kwa wagonjwa. Ndiyo maana tunachomwa chanjo mbalimbali kujilinda.
Tumejitolea maisha yetu kwajili yako, hivyo pindi upatapo shida tuone hasa kabla tatizo halijawa kubwa. TUPO KWAJILI YAKO.


Sekta ya Afya ni sekta yenye fursa nyingi sana. Kwasababu, utafanya yote lakini Afya itabaki kuwa sekta muhimu sana kwenye jamii. Fursa ni nyingi sana kupita maelezo. 
Asanteni.

8 comments:

  1. Kijana elim yako nimeelew na nazid ielewa daily God bless u ufike mbalii

    ReplyDelete
  2. hello.
    naomba nikusahihi she kidogo kwenye upande wa degree hatuna lab tech ila tuna lab scientist. wao huwa wana deal na kufanya intepretation for what is going on on the back of every process done in the laboratory.... but technicians wao kazi yao nikufanya kazi zilizopo kwenye maabara and most of them huwa hawajui the chemistry behind techniques.

    ReplyDelete
  3. Congrats bro!
    you are doing a great job

    ReplyDelete
  4. kuna hawa wanaoitwa physiotherapists...wanafit vipi kwnye sekta ya afya???

    ReplyDelete
    Replies
    1. Wanahusika na tiba kwa mazoezi ya viungo... Mfano mtu aliyepooza au mwenye matatizo ya uti wa mgongo, wanamfanyisha mazoezi kutibu kama ni maumivu n.k. Kwa Tanzania, sifahamu kwa undani chuo kinachotoa hiyo course.

      Delete