Wednesday 6 July 2016

NAFASI YETU KATIKA KUOKOA MAISHA KWENYE AJALI ZA BARABARANI

AJALI BARABARANI

Kwanza niwape pole wale wote waliowahi kupotelewa na wapendwa wao sababu ya ajali mbali mbali za barabarani. 
Ni ukweli usiofichika kwamba hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa sana la ajali barabarani. Tujiulize, wiki hii tu taarifa za ajali kwenye magroup yetu ya whats app tulizopata ni ngapi?
   
karibu tuzungumze sasa:
-Constantine Ntanguligwa(MD student Muhimbili university of health and allied sciences) 
-2030hrs 6th July 2016

Ajali ikitokea iwe ya pikipiki au gari kuna vitu vikuu viwili vinavyoweza kusababisha kifo. 
   1. Immediate death(kifo cha papo kwa hapo) due to severe head injury or trauma(kuumia sana kichwani ). Hii itapelekea kuharibu sehemu nyeti zinazokuwezesha wewe kufanya vitu kama kupumua au moyo kudunda.
   2. Slow death. Hapa ndo ile mtu anakimbizwa hospitali na mnakuja kuambiwa alifia njiani au hospitalini. Mara nyingi hii inatokana na kitu tunaita ,"severe haemorrhage" yani kuvuja damu sana hasa kutokana na rupture (kupasuka) kwa mishipa mikubwa au mikuu ya damu mwilini inayopelekea kupata kitu tunaita "shock". Mwili huitaji maji kuliko kimiminika chochote kile hivyo unapopata shida hii ndo maana unaongezewa maji immediately wakifika jamaa wale wa huduma ya kwanza. Na Ubaya hospitali zetu zinaupungufu sana wa damu salama ingawa wanaweza kukuwekea maji tu kama huduma ya kwanza.
  
Wito wangu kwenu watu wangu wa nguvu kama wahanga wakubwa wa hili, mvae helmet na seat bealts(mikanda), Kwa kiasi kikubwa hivi vimelengwa kupunguza hiyo severe head injury iwapo ajali itatokea. Helmet itakukinga na seat bealt itapunguza momentum(nishati) itakayotoka kwenye kifaa chako cha moto kwenda kichwani.

Nanukuhu shirika la Afya la umoja wa mataifa(WHO):
retrived 2017hrs 6th July 2016 http://www.who.int/mediacentre/factsheets/fs358/en/

Key facts
  • -About 1.25 million people die each year as a result of road traffic crashes.
  • -Road traffic injuries are the leading cause of death among young people, aged 15–29 years.
  • 90% of the world's fatalities on the roads occur in low- and middle-income countries, even though these countries have approximately half of the world's vehicles.
  • -Half of those dying on the world’s roads are “vulnerable road users”: pedestrians, cyclists and motorcyclists.
  • -Without action, road traffic crashes are predicted to rise to become the 7th leading cause of death by 2030.
  • -The newly adopted 2030 Agenda for Sustainable Development’s has set an ambitious road safety target of halving the global number of deaths and injuries from road traffic crashes by 2020.

Motorcycle helmets
  • Wearing a motorcycle helmet correctly can reduce the risk of death by almost 40% and the risk of severe injury by over 70%.
  • When motorcycle helmet laws are enforced effectively, helmet wearing rates can increase to over 90%.
  • Requiring helmets to meet recognized safety standards ensures that helmets can effectively reduce the impact of a collision to the head in the event of a crash.
Seat-belts and child restraints
  • Wearing a seat-belt reduces the risk of a fatality among front-seat passengers by 40–50% and of rear-seat passengers by between 25–75%.
  • Mandatory seat-belt laws and their enforcement have been shown to be very effective at increasing seat-belt wearing rates.
  • If correctly installed and used, child restraints reduce deaths among infants by approximately 70% and deaths among small children by between 54% and 80%.

  • Ajali haina kinga, haibishi hodi wala kutuma notification ndugu zangu hebu tufuate hiyo miongozo tuzingatie maisha yetu. Tunaweza kuokoa maisha yetu kwa kuchukua sekunde thelethini tu kuvaa mkanda au helmet.
  •  
  • Karibu kwa maswali.

2 comments:

  1. pia kitu cha 3,ajali hupelekea uharibifu wa mali e.g gari,nyumba n.k vilivyopo pembeni pindi ajali inatokea

    ReplyDelete
    Replies
    1. Safi sana. Asante kwa mchango wako ndugu.

      Delete